Wosia na Vitu vya Kuzingatia Wakati wa Uandaaji wake Tanzania
Utangulizi
Wosia ni nini?
Wosia
ni kauli ama tamko analolitoa mtu wakati wa uhai wake kwa hiari akieleza ni
nini kifanyike baada ya kifo chake,pia huonyesha nia yake jinsi gani mali zake zigawanywe baada ya kufa
kwake,katika wosia muusia anaweza pia kutamka ni wapi azikwe baada ya kifo
chake.
Aina za Wosia
Kuna
aina kuu mbili za wosia nazo ni;
i.wosia
wa maandishi
ii.wosia
wa mdomo(usio wa mandishi).
Wosia
wa maandishi ni wosia ambao huandikwa kw maneno katika karatasi na wosia wa
mdomo ni wosia ambao muusia haandiki wosia wake katika ila husema kwa mdomo tu,
Wosia wa Maandishi
Ili
wosia wa maandishi ukubalike kisheria lazima uwe na vitu vifuatavyo;
Uandikwe
katika karatasi nyeupe na uandikwe kwa kalamu isiyofutika yaani ya wino na si
ya risasi.Anayetoa wosia awe na akili timamu na ataje kama ana hakili timamu na
pia aonyeshe kama alitoa wosia kwa kwa hiari yake.Ushuhudiwe na mashahidi
wanaojua kusoma na kuandika angalau wawili (mmoja wa ukoo na mwingine mtu baki)
hii ni pale muusia anapokuwa anajua kusoma na kundika.Na pia kama muusia hajui
kusoma na kuandika ushuhudiwe na watu wanne (wawili kwa ukoo na wawili watu
baki).Wanaotarajia kurithi au watu wenye maslahi na wosia huo hawatakiwi
kushudia. Wosia huo usainiwe na muusia mbele ya mashahidi wake wakiona,akitia
saini yake na kama hjui kusoma na kuandika basi atie alama ya kidole gumba
chake cha kulia.Mashahidi pia watie saini zao.Mashahidi lazima wawe
wammechaguliwa na muusia mwenyewe.
Wosia wa Mdomo
Vitu vya kuzingatia wakati wa
kuandaa wosia wa mdomo
Ushuhudiwe
na mashahidi wanne (wawili wa ukoo na wawili watu baki)Mashahidi wawe
wamechaguliwa na muusia mwenyewe Muusia awe na akili timamuKama mashahidi
watakufa kabla ya muusia kufa basi wosia hautkubalika na urithi utagawiwa kadri
ya mpango wa urithi usio wa wosia.
Angalizo,wosia
unaweza kubatilishwa pale ambapo utatolewa bila kuzingatia mambo ya msingi.
Faida za Wosia
Muusia
anapata fursa ya kugawa mali zake kwa watu anaotaka wagawiwe.Wosia unaepusha
ugonvi na migogoro baina ya nduguMuusia anapata fursa ya kuamua ni nani awe msimamizi wa mali
zakeMuusia anapata fursa ya kuchaguaa azikwe wapi
Mahali pa kutunza wosia
Wosia
unatakiwa utunzwe sehemu salama,sehemu hizo ni kama benki,kwa
mwanasheria,mahakamaani au kwa mtu yeyote ambaye muusia anamwamwini.
Hitimisho,watu
wanashauriwa kuandaa wosia wakati wa uhai wao,watu waache uchuro hii ni
kwasababu wosia una faida sana kwa muusia na wale wanaobaki.
Marejeo,
Chama
cha wnasheria Tanzania bara

0 comments:
Post a Comment